Saturday, June 25, 2022

#KUMBUKUMBU NA NGUVU ILIYOFICHWA KWENYE MWANZO NA ASILI YA JAMBO

Kumbukumbu au memory (that faculty by which mind stores and remembers information) kwa mwanadamu yeyote ndio thamani yake, kama sio tazama kichaa, tahira au yeyote ambayo kifaa cha kumbukumbu (ubongo) kina dosari ama hitilafu fulani; thamani na umuhimu wake hupunguka ama kutoweka kabisa. Kuna nguvu katika kuwa nayo hata asili ya yote ni katika kukumbuka ndivyo uhuishavyo nguvu ya nafasi yako kiuungu na kimwili, na yeyote asahauyo hana umiliki wa chochote. Mungu ni wa kumbukumbu (Kumbukumbu 15:15), huwakumbusha wanadamu na kuwataka kukumbuka, na pamoja na mikasa yote tangia mwanzo na yote yaliyojiri duniani, Mungu alitunza maneno na matendo yake  kupitia watu wake aliowachagua na shuhuda zao kumhusu yeye kwa njia ya maandiko kwa kumbukumbu za umilele na yote yadumu mpaka leo...na Musa alijua bila kumbukumbu hakuna hifadhi ya asili ya kitu chochote ndio maana katika torati kuna kitabu alikidedicate kama kumbukumbu la torati. Najua ktk uandishi wake wa torati kuna kumbukumbu ya maandiko ya kale alikuwa nayo wakati Mungu anasema juu ya yapi ayaingize kwenye uandishi wa torati. Na kwake ilikuwa rahisi sababu katika ukoo wa lawi ndio ukuhani wa israeli ulidumu na hivyo walikuwa na historia yote ya mwanzo wao na mwanzo wa yote yaliyofunuliwa katika vizazi vyao toka asili ilivyokuwa na ikiwa rahisi kwao kujua Mungu huyu ni wa namna gani na ana abudiwaje. Hivyo uhodari wa taifa la israeli na nguvu yake i pia katika utunzaji wa historia na kumbukumbu zake, kama ilivyonguvu na uhodari wa malkia wa uingereza iliyokatika siri ya asili ya ufalme wake aijuaye yeye pekee mkaliaji wa kiti cha ufalme nayo i katika kumbukumbu za ufalme na pasipo yeye ufalme utayumbishwa hadi amrithishapo ufalme mmoja wa uzao wake na kumuasa kupitia kumbukumbu za kiti kile cha ufalme tangia mwanzo apate ufahamu, nguvu na hekima kuu ya utawala (na punde litajiri hili), ama kama ilivyonguvu na uhodari wa roman catholic ni vyote vyenye asili iliyodumu muda mrefu na kumbukumbu zake si rahisi kuviangusha na kuvishinda nguvu, vyenye asili ya muda mrefu vyahitaji muda mrefu kuvibatilisha kushinda nguvu zake kwanini kwa sababu kabla ya kushinda inabidi sio tu kujua asili yao bali kuifuta kwenye kumbukumbu zao na mioyoni mwao ili wasiweze tena kuwa hodari na nguvu kuu na kisha kuwashinda, mfano kwa RC likumbuke hili wenye uwezo wa kuibadilisha syllabus yake ni walioweza kuaccess asili yake walio katika level ya upapa na wafuasi watabaki kuwa wafuasi wa RC. Unajua pia hata mukuyu mkubwa miaka mia saba, mia nane nguvu yake ya miaka mingi ikatika mizizi yake roots ambazo zinahistoria kubwa ya kwamba iliwezekanaje ilishindaje na pia utaona mizizi yake ambaye ni uhai wake kuwa imara sana imeenda mbali sana na ni deep sana kwenye source of life' water na ndio juu huoni mukuyu ukitikisika kwa dhoruba yoyote sababu haujauacha uhai wake asili yake kabisa' water kule deep down ina mahusiano yadumuyo, na kwenye mizizi pekee ndio katisho la uhai wake lilipo, kwa hivyo aliyeijua mizizi yake na kuaccess deep down asili yake ana uwezo wa kukatisha uhai wake mkuyu mkubwa na fahari yake na hata kuibatilisha kwa maana ana siri kuu ya nguvu yake. Twajua nguvu ya kristo na umilele wake usioweza kufananishwa na yeyote, kutokana pia na kuweza kuestablish kudadavua asili yake kupitia kumbukumbu kuanzia adamu mpaka yeye na kisha kuithibitisha ile Yesu ni Bwana ni baada ya kuunganisha na kujua kumbe Bwana wa kutoka mwanzo ndio Yesu mwenyewe, no wonder mtume wa Yesu kristo (Mathayo 1) aliweza kuandika asili ya Yesu kutoka Adamu mpaka kufikia Yesu kupitia kumbukumbu. Siri ikiwa siri kuu kwa mwenye nayo hakuna aiwezaye nguvu yake itakuwemo mpaka pale ujulikanavyo ndipo nguvu yake ni rahisi kuififisha na kuishinda, na ndio maana Mungu hatumujui jumla ni kwa sehemu tu na hiyo ni kwa sababu anataka tuwe kama yeye japo kwa sehemu hiyo anayojifunua kwetu. Huwezi kuiteka nyara nyumba pasipo kumfunga kwanza mwenye nguvu ndani yake, na ili kumfunga lazima ujue kwanza siri zake na asili yake na hivi kama kumbukumbu hazipo na huna uwezo wa kuziaccess basi humuwezi kabisa. Na yeyote awezaye kuzipata kumbukumbu za asili yake na kuzielewa pamoja ikibidi kuzishinda huweza kufikia hatua ya kuwa na nguvu hizo kuzifuata ama kuziovertake na kuanzisha kitu kipya kipinzani juu yake. Wakati afrika inatakiwa kutawaliwa kuifanya nyara yao wakoloni walitumia njia nyingi na zote zilikuwa na maana kama ya mamisionari kabla ya kujiaminisha kuja kupambana ili kuwateka waafrika. Explorers na Wamisionari pamoja mengine walitaka kujua kwanza asili yetu ambayo ni nguvu yetu na walitumia kila falsafa ili kujua hilo walivyojua kwa sababu pamoja na kumbukumbu lakini yalikuwa mioyoni mwao na kila kabila lilihakikishwa kwenye kila kizazi kuna mtunza kumbukumbu atakaye zihamisha kwenda kizazi kingine kipya cha damu yao (kabila) na kuhakikisha yote ya kale yanaeleweka na yanatunza mioyoni mwao kwa maana ndio nguvu yao. Kuna msemo unasema mali bila daftari hupotea bila sababu, hivyo basi kabila bila kumbukumbu hufutika na kisha kupoteza asili na kuanzishwa kitu kipya, sasa kupotea kwake hakuondoi gharama ya kupotea huko, waliopotelewa na kumbukumbu ya asili lazima wagharamike sababu mwenye asili yupo naye atakuwa na kisasi na kila abezaye na kudharau kwa kusahau kabisa uwepo wake iwe kwa kusababishwa na wengine ama wenyewe. Hivyo basi hao wamisionari wakatumia nguvu kubwa baada ya kujua kuhakikisha wanazifuta kumbukumbu zetu pamoja na vile vilivyoashilia miungu yao kuviteka na kuviondoa kwao na kisha kuifuta mioyoni mwao na akilini kwa kuwapa elimu na utashi wa kibiblia wawe wapya kwa yote na zidi unavyosimama katika utashi huu mpya unafuta ule wa kale na kumbukumbu zake. Akutakaye kuwa na nguvu juu yake atakupa kujua asili yake na kumbukumbu zake utajua siri yake na hivyo utakuwa na nguvu za kuishindaniya nafasi yake hata ikibidi kumshinda ukiweza. Siri za Mungu alizomfunulia shetani ndio zilizompa lukwale' uwendawazimu wa kuitaka nafasi yake na kumbukumbu za siri hizo ndipo ilimo nguvu ya ufalme wake. Adamu wa pili alihuishwa katika Yesu' na kwa kuwa adamu alifanywa muumbaji wa dunia hii na mungu wa dunia hii na mwenyezi Mungu, hivyo Yesu alikuja kututekea nyara ufalme wa adamu uliopotezwa naye na hivyo mwana wa adamu kuishi pasipo huo. Watawala wa dunia huact kama mawakala wa mungu wa dunia hii kabla ya Yesu kufunuliwa maishani mwako, na ndivyo alimpasa kufa, sababu alikuja kumfanya kila mtu mungu wa dunia hii, muumbaji mdogo na hata aliyeko chini sana aliyedharauliwa ili litimie yeye ni Mungu wa miungu yote ya jamii yake isiyokengeuka ya ufalme wake na wote tuiishi ahadi ya neno hilo, kwa kuwa shetani baada ya kumzidi adamu akili na kutawala dunia kama mungu sehemu yake adamu, mawakala wa utawala wake hawakumruhusu Yesu kuinuka kama Mungu (baada ya kutukuzwa) na mfalme juu yao wote hivyo wakamuua na hivyo kifo chake haikuwa tu kuhusu taifa la israeli bali mamlaka ya dunia yaani shetani aliyejitukuza duniani katika sehemu na nafasi ya adamu wa kwanza (mawakala wake walitenda kazi ile kujaribu kuzima ufalme; hila za namna hiyo zimewaangusha kina ghadafi, falme za irani kwa kudai washikadau ndio wamemuua mkuu wao kumbe ni fitina za mamlaka za dunia kuangusha fahari ya mamlaka iliyopo kuwafaidia wanadaiwa na kuwa walengwa walioiangusha). When war is of gods only gods know the really course and the source and not others, vita iwapo ya miungu ni miungu pekee ijuayo kisa mkasa na kwanini na siyo washikadau au wafaidia miungu hiyo, wao hao wanaweza kujua baadae kwa sehemu kwamba kwa nini kutokea kilichotokea?.

Yote haya nayasema kuhuishwa umuhimu wa kumbukumbu na nguvu ya chanzo ama asili. Mwanadamu yeyote hawezi kuvishinda vifungo vyote alivyofungiwa pasipo kujua hivyo vifungo na pengine kama kweli vipo na vimemfunga. Kujua chanzo kunampa mtu kuwa na mkakati wa kujitoa kwenye mkwamo wa muda mrefu na miaka mingi. Kujua chanzo ni kujua siri ya kwa nini upo hapo na je ni hapo ndio unapasa kuwepo ama umefungwa nazo kumbukumbu zitakufanya ujiassess vizuri kwa kuangalia historia na mwenendo wake ndipo utapata nguvu ya kupambania hatua mpya zaidi na kutoka kwenye mkwamo huo. Vifungo vipo sana tu kwa mwanadamu na ndio maana hata Yesu mwenyewe anasema njooni kwangu nira yangu ni raini na mzigo wangu ni mwepesi hata ajae kukusaidia sharti aweze kukufunga ili uambatane naye kiroho na kimwili na hivyo basi vifungo kwa mwanadamu ni lazima dunia ilishavamiwa na mvamizi shetani awafunga wenye nayo dunia sababu alishamfunga kwa kumzidi akili mungu wa dunia hii adamu, na hivyo miili yetu ni kama imesetiwa kuangukia kwenye vifungo hivyo vyenye dhambi ya asili, na hiyo yote ili mwanadamu asijitambue kuwa yeye ni mungu wa dunia hii na shetani anainjinia vifungo hivyo kupoteza ufahamu huo ili usikumbuke ama kujitambua nafasi yako ya asili mungu wa dunia hii kwani chanzo hicho kitakujuza wewe nguvu yako juu yake hivyo haliruhusu hilo akiwa amekaa kwenye nafasi yako ya umungu wa dunia hii japo itifaki ya mwenyezi Mungu hata shetani pamoja na kukalia nafasi hawezi kuitangua ya kwamba dunia itatawaliwa na mungu adamu na wana wake na yeyote atakaye kuitawala hata kwa hila ni sharti amutumie adamu na wana wake, no wonder' Mungu kuurejesha ufalme ilimpasa aje kama adamu wa pili sasa, naye shetani anatupofusha kwamba usimamapo nafasini mwako kwamba unajitukuza kwa kukukosesha na wanadamu wengine ili ubaki chini kama walivyo wengine na yeye abaki kuwa mungu pekee wa dunia pasipo haki sababu hana mwili wa kutawala kihalali kama mungu wa dunia ya adamu na wana wake.
Ee' mwana wa adamu funguka adamu baba yako asili ya damu zote alifanywa mungu wa dunia hii, baada ya kukosea Mungu mwenyezi kupitia Yesu' yeye aliyefanyika adamu wa pili alikuja kuuhuisha ule ufalme ili wana wa adamu wabaki kuwa miungu ya dunia kwa kuwa aliona mateso na kukandamizwa kwetu na shetani na kwa kudhulumiwa haki yetu ya utawala wa dunia yetu wenyewe kama miungu, ifanye leo ahadi ya Mungu juu yako mwenyewe itimie kwake (Zaburi 82:5-7) ee! mungu wa dunia hii we sio wa kawaida kama unavyojichukulia mkubali Bwana leo hii akuokoa kisha akupe roho wake akujuze zaidi uyapasayo kutenda kama mungu wa dunia, hivi kama Mungu mwenyezi ameamua mwenyewe kujimultiply kwa wana wake (sons of God) waliowashindi katika yeye, wewe ni nani hata upinge? wewe ni nani hata ukatae? Nasema wewe ni nani hata useme hapana?, jambo hili litasimama hakika na kweli yake aliyoiinua kupita jina lake lote hiyo ahadi yake itatukuzwa milele yote. Asema ili mapenzi yake Mungu wa miungu yatimizwe duniani kama vile yatimizavyo mbinguni, mwana wa adamu wewe uliyezao la damu hakika katika asili yako ifanyikavyo uumbaji tumboni mwa mama, wewe ni mungu wa dunia hii na damu yako yashuhudia haya ya kwamba ni mungu wa dunia wewe! ule uhai wake ndani yako damuni. Jua hekima hii ya kidunia chai iliyopoa ili kuhuisha joto lake inakupasa kumimina chai ya moto ya jamii ile ya mwanzo kulinda hadhi na uhalisia wake, na uhai wa damu iliyopunguka hulindwa na kumiminiwa damu mpya nyingine ya asili ya mwanzo kuhuishwa kwa upya vya asili ya mwanzo huku ikiweza kubatilishwa vimelea vya magonjwa, udhaifu na upungufu wowote uliokuwemo kwanza. Hivyo basi kukurejesha nafasini mwako kama mungu wa dunia hii ilimugharimu Mungu kumimina damu mpya kuhuisha damu ya adamu wa kwanza iliyofitinisha uungu mmoja wa mwanadamu na Mungu baba wa mbinguni ili ufalme mmoja naye udumu duniani kama ilivyo mbinguni, ni mapenzi yake hayo hiyo yatimize kwa kukubali kumpokea ili nafasi yako kwa mwana wa adamu wa pili ihuishwe ndani yako kupitia yeye Yesu' adamu wa pili aliyeshinda yote na akamnyang'anya mamlaka yako shetani aliyokuibiwa wewe na kukupa wewe tena hivyo okoka ili uishi kama mungu wa dunia hii hiyo ndio mara mia yako itakayoipata katika dunia hii na kisha uzima wa milele yaani huo ufalme wa Mungu duniani kuwa kweli mfalme. Shetani anatembelea nyota yako, namna manual ya kuwa mtawala na mumiliki wa dunia hii kama mungu wa dunia hii anatembelea shetani yaani ile baraka ya uadamu japo ameweka na mapotofu mengi ili usiifikie' amua leo mfuate Yesu atakujiza tu, naye shetani kama alivyoandikiwa na kuamuliwa kama adhabu yake ya uasi atakusujudia wewe uliyemdogo na punde kufanyika mkuu kuliko malaika, sababu shetani aliyekuwa malaika mkuu akusujudia wewe aliyemwamini Yesu na kuokoka. Jitambua leo mungu hanaga hofu wala woga ni jasiri katika njia zake, ni mungu wewe jitambue sasa Baba yako aliyeko mbinguni amekutukuza katika dunia na fahari yote ya dunia uimiliki na uitawale wala siyo shetani.
Arise and takeover the earth, oh! man as a god of this earth of which you are his/her product. i.e. created from it to be above it and not other but only you. Wewe uliyesehemu ya dunia, mwana-damu, mwana-nchi, mwana-udongo, mwana-ardhi hii tawala, tiisha vyote kwa uungu wa Mungu ndani yake ungali na nguvu, hata pale mwili utapoexpire nao utaenziwa ardhini, heshima ya mwili ni udongo na udongo ni sehemu yako uweza wa uumbaji wa vya jamii ya udongo u mikononi mwako kwa kinywa chako umba vyote navyo havitaacha kudhihirika kwa ajili ya utukufu wa Mungu wa miungu. Nasema Amka' uinuke juu uangaze kama mungu wa dunia hii, selah!!!. Ukiamini utaiona baraka hii na kuiishi, kita mizizi duniani na uitawale kama dunia kama mtawala halali wa sehemu yako. Kuna waliyojitambua hata sasa ambapo mtu aiishi ahadi ya kuwa taifa teule na mzao wa kifalme na ni wana wa adamu wenzetu ambao wanakuwa na wengine wanaenda kuwa na status ya kufanyika kama taifa katika nyakati hizi za sasa hali ni mwana wa adamu kama wewe sizungumzii nyakati za yakobo kufanyika taifa la israeli yamkini kipindi kile wakati ulicheleweshwa sana ahadi kutimia lakini katika Kristo Yesu wakati umekombolewa sana ukiwa ndani yake ni punde tu mwana wa adamu mmoja kuwa taifa teule na kuiishi ahadi ya Mungu na dunia kumutambua kama taifa ndani ya dunia ni nyakati za mwisho hizi, ni nyakati za miungu ya jamii ya Mungu mwenyezi, Mungu baba kuitawala dunia tena na sio tena mizimu iliyoimtii shetani na kuwa mawakala wa utawala wake usio na haki yoyote, hivyo funguka na ujitambue wewe sio kuku ni tai, wewe sio panzi ni jitu tena ni jitu la kutisha falme zote za ulimwenguni anazotawala shetani pasipo haki ya utawala, kwani ujionavyo wewe mbele zao ndivyo walivyopaswa wao kujiona hivyo mbele zako wewe mungu wa dunia hii. kumbuka tu hii neno la Mungu lasimama milele na ahadi yake ni kweli na amina.