Thursday, April 7, 2022

#UHALISIA WA UHALISI ama UHALISI WA UHALISIA'

Kibinadamu iko hivi, kwa mfano; Level ONE: Mbariki_blesser; ni abarikiye wengine...sio ndio!!,

Level TWO: Mbarikiwa abarikiye _ blessed blesser; anakuwa ni anayebariki wengine naye huku akibarikiwa, yaani mrithi baraka (1 Petro 3:9).


Hivyo ni sawa na yafuatayo;

Level ONE: Mvurugaji _Confuser; anayevuruga wengine na vya wengine....

Level TWO: Mvurugaji mvurugwa_ confused confuser; anayevuruga wengine avurugwaye naye.


Level ONE: Mharibu_ destroyer; aharibuye...

Level TWO: Mharibu mharibiwa_ destroyed destroyer; aharibuye aharibiwaye.


Unaweza endelea na wewe kuyadadavua mengine, mfano; mchonganishi, mfitini, mtapeli,  muongo, muangushaji (m-let down), muonevu, msahaulifu, mkwamishaji, mpuuzaji, mnyimaji, mtoaji, mdharauji, mpaji, mchukiaji, msaliti, mpendaji, mropokaji, mbinafsi, mkali, mkarimu, mtaratibu, mtengaji, mdhulumaji, mchochezi, mchonganishi, mchongezi, mlalamikaji, mlalamishi, mhukumu, mzinifu, mlaaniji-cursing person, etc.

Sasa ukifika level TWO wewe ni brand, unayobanner kabisa kwa eneo lako yaani wewe ni weapon. Katika yote mtu huhusika katika kuiendeleza au kuboresha hulka ama silika ama wengine huita haiba iliyoko na wengine huiunda hata ambayo haikuwepo kwanza kutokana na mazingira walioishi.

《《LUKE 6:38》》

Kila tabia na kikombe chake, usiwe kama yule wa Zaburi 109:17-19, usipende vya giza kuliko vya nuru venye utukufu ( Yohana 3:19, Zaburi 52:3), kuwa kama Yesu Kristo, mpenda mema mtenda mema.

///Psalm 34:14/// 

Hata hivyo karibu kwa NEEMA na REHEMA, anayamudu haya, mwenye hiyo atakubadilisha, ataihuisha roho yako kwa upya!!....

...kutana na GOD of Grace & Mercy!...

...kisha uwe kama Warumi 8:5.....