Sunday, August 25, 2024

#U MWANA WA MUNGU

 


Somo  la  Yesu kwetu ni nini?

Uwana wa Mungu ni uwakilishi  wa Mungu Baba aliyeketi ktk kiti cha enzi, kama yeye alivyo mbinguni  ndivyo nasi tulivyo  duniani (Wakolosai 2:9-10, Waebrania 1:1-10).

Na usiwe na shaka kuhusu hili kwani kuna haki hiyo (Yohana 1:12-13).

Sasa ktk Mathayo 16:13-20; pale kaisaria-filipi ndipo ilifika hatua na saa ile ya Yesu kufunuliwa kama mwana wa Mungu ambao huo ufunuo ndio mwamba wenyewe ambapo kanisa limejengwa kiroho na imani yetu ktk yeye inasimamia hapo.

Ule ufunuo kupitia Petro saa ile ( peter confession), ule uthihirisho  na uthibitisho mkuu wa Yesu  Kristo pale kaisaria-filipi  alipokuwa amekaa  na mitume chini ya miti  ya miforsadi (mulberry), ndipo ulipo weka msingi na maana kuu ya huduma yake  duniani. 

Katika hatua zote za  maisha  ya Yesu  duniani,   wakati akisubiri  kufunuliwa   kwake  mioyoni  mwa  watu ile saa  iliyokusudiwa   na Mungu  baba, ukamilifu wake ulifikiwa kwa watu kumuelewa  yeye aliye mwana wa adamu kama mwana wa Mungu, na ilimchukua muda kueleweka hivyo sababu ufahamu wa binadamu unachelewa kuchanganya (slow to wit) inapokuja kuhusu  mambo ya rohoni, na hiyo ni kweli.

Yesu alipita stage ya utoto kama mwanadamu wa kawaida (conscious inakuwa dimly ktk kujitambua), then ya pili ya kujitambua,  roho anaanza kujifunua ndani yake ktk ujana na mpaka ukubwa wake (pale conscious iko light-up, anakuwa aware mambo mengi ya divinity na mission yake), ya tatu ni ubatizo, kujithihirisha kwa Mungu kwake  kama mwanae  na kuanza huduma  kama  mwalimu wa ufalme wa  Mungu, then mwalimu na mponyaji, hapa watu wa karibu walimjua kama mwana  wa  adamu na wengine wakamuita mesia, wengine  wakataka  hata  awe mfalme wa wayahudi, na  stage ya 4 na ya mwisho ilianzia  pale kaisaria-filipi alipofunuliwa  kama mwana wa Mungu na mpaka kusulubiwa kwake na kifo cha msalaba, na  ktk stage  zote hizo Yesu hakujikuza bali ulikuzwa  kwa namna alivyokuwa anaishi, its stages  kama ukuaji  wa kipepeo  kutoka buu, its  marked the new start  when  was observed change supernaturally organically.

Can you  be the son of God? Unaweza kuwa mwana wa  Mungu?

Yes! nasema unaweza kuwa mwana wa Mungu leo, kupitia  kumwamini kristo kama  Bwana  na  mwokozi wa maisha  yako.

Haya basi, nawe mwana wa Mungu  mwenye haki  kwa  roho wake mtakatifu kupitia ile imani ktk kristo   Yesu (Wagalatia 3:26), ktk kujitambua kwako hivyo pokea funguo za mamlaka  kuyatenda yaliyo makuu duniani kama  mbinguni, na huku sifa kuu ya umwana ya kuyatenda yaliyo mapenzi ya Mungu Baba, hata yawe magumu vipi iwe ni jadi yako, naye Mungu Baba akuwezeshe pale uyatendapo hayo mapenzi yake (Yohana 5:19; Luka 22:42-43) 🙏🏾.