Tuesday, October 15, 2024

#UFALME WAKE, UFALME WETU


Luka 12:29-32 inashangaza sana, Yesu anasema; "Msiogope! enyi kundi dogo, kwa kuwa Baba yenu ameona vyema kuwapa nyie huo Ufalme". He said; "It's your Father's good pleasure to give you the Kingdom."

Hata Daniel 7:27 alitabiri kwa habari ya wana wa Mungu akisema; "Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii".
Tena katika  Yohana 17:22 Yesu anasema; "Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo na umoja".  ona He said; "that  glory which  you gave me, i  have given them", this is  powerful!
Sikia hii; aliteswa tupate haki ya kuwa na kuitwa wana wa Mungu.
Iliyoitwa kufuru kuwa mwana wa Mungu  ikawa haki yetu.
Kwa uthubutu wake, akagharamia hata mauti yake, alitamka hivyo ikawa.
Na haki hiyo ilikuja na uweza uliotupa sisi ujasiri na nguvu katika ukiri wetu kuwa sisi ni wana wa Mungu hakika.

Ilimchukua yeye kuishi kama sisi ili tuupate ufalme wake (Wafilipi  2:6-8); yeye mwenye namna ya  Mungu  toka  mwanzo alichukua namna ya  mtumwa akawa na mfano wa  wanadamu halafu alijinyenyekeza sana akawa mtii mpaka mauti, naam, mauti ya msalaba (kwani ilikuwa laana mtu kuangikwa msalabani-Wagalatia 3:13-14), Yesu anasema jina lako Baba litukuzwe duniani (Yohana 12:28, 17:4,6), kwamba kuitwa kwetu sisi wana wa Mungu ni utukufu kwa Mungu Baba.
Fikiria jina lake la heshima; imeandikwa  ktk Wafilipi 2:9-11 kwa jina hilo kila goti lipigwe la vitu vyote vya mbinguni, duniani na kuzimu.
Halafu, alizaliwa nalo kikawaida kabisa, kipindi kingine alikimbizwa nalo kwenda kufichwa Misri, aliishi nalo mitaani, alicheza nalo na hakuna aliyejua, saa ilipofika akajifunua kwalo hakuna aliyemsadiki, alikataliwa nalo, akatukanwa nalo, akatengwa nalo, makanisa yakamuhukumu nalo, akateswa nalo, akasulubiwa nalo, kufa nalo msalabani na kuzikwa  nalo.
Hii yote kwa ajili yako wewe na mimi,   kwani hakuwa tayari kuona sisi tunanyanyaswa kwa kuwa gizani kuishi isivyotusitahili asili yetu, kwa hivyo siku ya tatu akafufuka nalo, halelujah! ili tu sisi tukamilishwe kwalo, tuitwe na tuishi kama wana wa Mungu, wana wa ufalme wa mbinguni  duniani. Bwana Yesu asifiwe!..
Chukua nafasi hiyo sasa, kaa hapo, angaza, barikiwa, occupy till when He come again. Indeed; you are the son/daughter of God, amen.

Saturday, October 12, 2024

#THE TRUTH CO-ORDINATED LIFE

Truth co-ordination among brethren complete the mind of christ in us. Living the truth co-ordinated life perfect our righteousness in God.

~1 Corinthians 2:16🙏






Tuesday, October 8, 2024

#HABARI NJEMA KWAKO!



Make Holy Spirit count on you,

Jesus Christ proud, 

The Almighty Father smile and,

All the Heavens  rejoice.

It's New Dawn now.

Thanks God 🙏🏾.


*Kukuwa katika imani ni pamoja na kutochanganyikiwa ktk semi hizi mbili👇🏾 kwa maana Kiti cha Enzi ni kimoja na Mungu aketiye juu yake ni mmoja tu, Baba wa Mbinguni*

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Mfanye Roho Mtakatifu awe nawe 🫵🏾,

Yesu Kristo aone fahari, 

Baba mwenye enzi yote atabasamu,

nazo mbingu zikufurahie.

Ni mwanzo mpya,

Mshukuru Mungu.


~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Mfanye Roho Mtakatifu katika jina la Yesu Kristo  aone fahari kuwa nawe,

yaani, Baba mwenye enzi yote atabasamu katika utukufu wake,

nazo mbingu zikufurahie.

Ni mwanzo mpya,

Mshukuru Mungu.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ok!, ni kama kusema kwa mfano mzee mmoja mbobezi katika tukio la mafanikio ya mwanae katika uhasibu wake baada ya kusikia na kuona matukio yake ya kipindi chote ktk video, huku akiwa na moyo wa furaha alipopewa mic aseme neno akashusha pumzi kubwa na kusema;

 "Hakika kwa roho wewe ni roho yangu kweli kweli ni ndani yako mimi, kama mhasibu mi pia, najivunia sana wewe na kama Baba nimefurahi na kufarijika sana kwa mafanikio yako, na boma yetu yote wafurahi na kuwa na shangwe kuu kwa ajili yako, ni mwanzo wako mpya tena huu nishukuru sana mimi. Ni mimi Yoshua."


Ni Habari njema?,

Ndiyo! ni njema kweli hizi🙏🏾

Thursday, October 3, 2024

#HOLY GHOST [ROHO MTAKATIFU]


God's  Way not mere talk, it's an empowered life; living by God's power.

Ndio!, Ufalme wa Mungu ni nguvu ktk matendo na sio maneno sana (power in  action)~1Wakorintho4:20.

Matendo 19:1-20; Neno la Mungu la ufalme (kingly word of God) lilizidi  kuenea  Efeso na kushinda kwa nguvu, sababu  ya  nini? uthihirisho wa  Roho  Mtakatifu. 

Sasa kama ni majivuno kwa mkristo yeyote, ni kwa  sababu ya kumpata Roho  Mtakatifu, ambayo ni neema kubwa sana.  Waliomsikia Yohana  mbatizaji Neno linasema  waliamini neno la  toba wakatubu na  kubatizwa ikaishia hapo, ila ktk  Yohana 1:12 kwa waamini  wote wa Yesu kristo Mnazareti, aliwapa uwezo  wa   kufanyika watoto wa  Mungu,  ule  uwezo ndio nguvu iletwayo na Roho  Mtakatifu.

Na je' sasa we ni  mwamini wa  Yohana  Mbatizaji ama wa Yesu Kristo wa Nazareti?  Jiulize!

Mwana wa Mungu kama  kweli ndiye,  son/daughter of God, omba uwe na Roho  Mtakatifu, hapo  inaleta maana ktk imani yako, na asiwe anaheri   mpagani kukuzidi, naye  huyo Roho akiwemo ndani yako atajithihirisha nawe utakiri kweli sasa ninaye.

Mfano mzuri ktk kizazi  chetu  mwanzoni mwa miaka ya 1900s, Mwafrika  mweusi  William J.   Seymour, mtumishi wa  Mungu huyu aliyekuwa  kipofu jicho  moja hakupendezewa na imani butu, alitamani  matendo ya  mitume yaendelee na aliamini kuwa kunena kwa lugha ni ishara mojawapo ya  mtu  kumpokea Roho  Mtakatifu (Holy  Spirit Baptism), akawa na  shauku sana kila  akisoma  Matendo 2:4, shauku hiyo ikampelekea kuwa na  mzigo kutaka kupokea na  hata  baada ya imani  kujaa aliokuwa  akiwahubiria wakaanza kupokea na kisha naye  akajazwa Roho Mtakatifu miaka ya  1914, na ndio ulipozaliwa uamusho wa Roho   mtakatifu  kwenye  mitaa ya  Azusa  ya Marekani, mpaka mitaani  watu wakawa  wanajazwa wanalewa  Roho Mtakatifu na kuanza kunena  kwa lugha  mpya, na huo  ukawa  mwanzo mpya tena wa upentekoste  kuenea  kwa  kasi baada ya kanisa  kupoa kwa muda na huduma nyingi zikaanza utume duniani kama Assemblies of God iliyoenea duniani kwote, nawe unajua kama hapa Tanzania  huwezi zungumzia mwanzo wa  upentekoste bila kutaja Tanzania Assemblies  of God (TAG), lakini jua ilianza na shauku ya mtu  mmoja,  hii ikithibitisha  kuwa Mwana  wa Mungu kweli  akiwa na Roho Mtakatifu ni Kuhani wa Kifalme na Taifa  teule🙏🏾.

so,

#Receive Holy Spirit

#Live like King, talk like Him

#Kingly virtues.

#Serve the Almighty God

Sunday, August 25, 2024

#U MWANA WA MUNGU

 


Somo  la  Yesu kwetu ni nini?

Uwana wa Mungu ni uwakilishi  wa Mungu Baba aliyeketi ktk kiti cha enzi, kama yeye alivyo mbinguni  ndivyo nasi tulivyo  duniani (Wakolosai 2:9-10, Waebrania 1:1-10).

Na usiwe na shaka kuhusu hili kwani kuna haki hiyo (Yohana 1:12-13).

Sasa ktk Mathayo 16:13-20; pale kaisaria-filipi ndipo ilifika hatua na saa ile ya Yesu kufunuliwa kama mwana wa Mungu ambao huo ufunuo ndio mwamba wenyewe ambapo kanisa limejengwa kiroho na imani yetu ktk yeye inasimamia hapo.

Ule ufunuo kupitia Petro saa ile ( peter confession), ule uthihirisho  na uthibitisho mkuu wa Yesu  Kristo pale kaisaria-filipi  alipokuwa amekaa  na mitume chini ya miti  ya miforsadi (mulberry), ndipo ulipo weka msingi na maana kuu ya huduma yake  duniani. 

Katika hatua zote za  maisha  ya Yesu  duniani,   wakati akisubiri  kufunuliwa   kwake  mioyoni  mwa  watu ile saa  iliyokusudiwa   na Mungu  baba, ukamilifu wake ulifikiwa kwa watu kumuelewa  yeye aliye mwana wa adamu kama mwana wa Mungu, na ilimchukua muda kueleweka hivyo sababu ufahamu wa binadamu unachelewa kuchanganya (slow to wit) inapokuja kuhusu  mambo ya rohoni, na hiyo ni kweli.

Yesu alipita stage ya utoto kama mwanadamu wa kawaida (conscious inakuwa dimly ktk kujitambua), then ya pili ya kujitambua,  roho anaanza kujifunua ndani yake ktk ujana na mpaka ukubwa wake (pale conscious iko light-up, anakuwa aware mambo mengi ya divinity na mission yake), ya tatu ni ubatizo, kujithihirisha kwa Mungu kwake  kama mwanae  na kuanza huduma  kama  mwalimu wa ufalme wa  Mungu, then mwalimu na mponyaji, hapa watu wa karibu walimjua kama mwana  wa  adamu na wengine wakamuita mesia, wengine  wakataka  hata  awe mfalme wa wayahudi, na  stage ya 4 na ya mwisho ilianzia  pale kaisaria-filipi alipofunuliwa  kama mwana wa Mungu na mpaka kusulubiwa kwake na kifo cha msalaba, na  ktk stage  zote hizo Yesu hakujikuza bali ulikuzwa  kwa namna alivyokuwa anaishi, its stages  kama ukuaji  wa kipepeo  kutoka buu, its  marked the new start  when  was observed change supernaturally organically.

Can you  be the son of God? Unaweza kuwa mwana wa  Mungu?

Yes! nasema unaweza kuwa mwana wa Mungu leo, kupitia  kumwamini kristo kama  Bwana  na  mwokozi wa maisha  yako.

Haya basi, nawe mwana wa Mungu  mwenye haki  kwa  roho wake mtakatifu kupitia ile imani ktk kristo   Yesu (Wagalatia 3:26), ktk kujitambua kwako hivyo pokea funguo za mamlaka  kuyatenda yaliyo makuu duniani kama  mbinguni, na huku sifa kuu ya umwana ya kuyatenda yaliyo mapenzi ya Mungu Baba, hata yawe magumu vipi iwe ni jadi yako, naye Mungu Baba akuwezeshe pale uyatendapo hayo mapenzi yake (Yohana 5:19; Luka 22:42-43) 🙏🏾.