#KATIKA KRISTO KUWA TOWASHI WA KIROHO KWA AJILI YA UFALME WA MBINGUNI

Biblia inasema katika Mathayo 19:11-12; Yesu akawaambia “si watu wote wanaoweza kupokea neno hili, isipokuwa wale tu waliojaliwa na Mungu. Kwa maana wengine ni matowashi kwa sababu wamezaliwa hivyo, wengine wamefanywa matowashi na wanadamu na wengine wamejifanya matowashi kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea neno hili na alipokee.

Muundo wa Kitowashi; Nabii wa Zimbabwe kwenye mahubiri yake haya alisema kanisani kwake kulikuwa na dada mmoja ambaye alifunga na kusali kwa siku 29 mlimani, ambapo kanisa limekuwa likiutumia huo mlima kwa kufunga na sala. Sasa huyo dada baada ya siku 29 za mfungo ambao ulimuweka katika hali ya kufa kabisa, yeye alikiri kuwa alifanya hivyo kwa ajili tu ya Nabii wake awe salama pamoja na yeye kujua jambo lolote ambalo lingeweza kumtokea baba yake wa kiroho (Nabii).
Kuna towashi katika neno la Mungu; towashi ni yule mtu aliyehasiwa ambapo hawezi tena kujizalisha yeye mwenyewe, hawezi kuwa na watoto yaani hakina kizazi kitakacho fuata baada yako. Yesu alisema kuhusu aina ya matowashi; kwamba wapo waliozaliwa matowashi toka tumboni wa mama zao, pili wapo waliofanywa matowashi na wandamu wenzao na pengine kwa kulazimishwa na aina ya tatu ni ile ambayo nataka kuiongelea haswa ambayo Yesu alisema wapo waliojifanya wenyewe matowashi kwa ajili tu ya ufalme wa Mbinguni, na Yesu mwishoni akasema yeye atakaye kupokea na apokee, kumbuka pia maneno ya Yesu mwanzo alisema lile nalokwenda kusema yaani kuhusu matowashi ni wachache tu watalielewa.

Sasa ukiangalia namna vile hapo kale na taratibu zao zilivyokuwa, utagundua na kuanza kuelewa ya kwamba matowashi walikuwa ni watu wa kuaminika sana kwa wafalme. Kila mfalme alihakikisha ana towashi katika makazi yake ya kifalme na ni matowashi tu waliokuwa wanaaminika na ukiwauliza wafalme kwa nini walipenda kuwa na towashi kuliko hata walinzi au mwanadamu yeyote, atakwambia nina mabinti kwenye ufalme wangu, vijana, wake ambapo hakuna mkorofi yeyote atakayetakiwa kuwaharibu mbele yangu ni towashi pekee anafaa nafasi hiyo. Hii ndiyo sababu pekee iliyofanya matowashi waaminike sana, walikuwa wanajaribu hata mvinyo wa mfalme kabla hajanywa ili kama kuna kitu kibaya kiwapate wao, matowashi hawakuogopa kufa kwa sababu hawakuwa na chakuishi hapa duniani isipokuwa kuwatumikia mabwana zao, wafalme. Na hii ndio sababu pekee ya matowashi kuaminika zaidi ya wale watu ambao walikuwa tayari kuzaa na kujizalisha wenyewe.

Siku hizi utaona mtu wa Mungu analia sio kwa sababu anakosa washirika wa karibu wa maono yake sio! kwani kuna watu wengi wanamzunguka karibu naye, lakini tatizo ni kwamba wakati mtu wa Mungu anataka kujizalisha na wao wanajizalisha kisiri na hiyo inaleta mvurugano baina yao kwani maono yanakinzana na kufitiniana. Katika biblia Mwanzo 14:14 inasema Ibrahimu alikuwa na wajakazi 318; waliofunza vyema kwa vita, jeshi ambalo lilikuwa lake mwenyewe la nyumbani kwake, lakini katika Sura ya 15 Ibrahimu anamlilia Mungu ya kwamba amemuacha na ya kuwa kwanini yeye hana mtoto, kwa hivyo unaweza kuwa na watu wengi  wanakufuata na huna mtoto hapo, kwa kuwa tu wafuasi wako wako kama watumwa na watumishi kwa hiyo kilio cha mtu wa Mungu kwa Mungu hakitaisha kitaendelea milele mpaka tu watu wa Mungu watakavyoweza kuzalisha watoto wakike kwa wakiume makanisani, kwa sababu tu watumwa au watumishi sio wana (kwani hawawezi kutunza maono yale yaliyo moyoni mwa mtu wa Mungu).

Sipaswi kujizalisha kwa namna yangu, lakini baba wa kiroho anapaswa kuweka mbegu katika mfumo wangu wa uzalishaji na mimi kuzalisha mbegu ya baba yangu wa kiroho, kwa hiyo kuna hatua ambayo ninapaswa kuwa kama towashi wa kiroho kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Kama tu Baba wa kiroho ataniamini ninapaswa kila siku kuangalia mfumo wangu wa uzalishaji. Ngoja nielezee vitu vichache kwa kina hapa; Wakati Mungu amemwita Musa, alikuwa na ufahamu kuhusu suala la wana Israeli huko Misri na usisahau kuwa kwa Israeli kutoka Misri alitakiwa nabii, lakini Israeli walikuwa wakiomboleza katika kazi za kitumwa huko Misri. Na ujue ni rahisi sana kuwa maskini lakini inakuhitaji uwe na nabii kutoka katika hali hiyo, kuna vitu ambavyo unaweza kufanya wewe mwenyewe lakini unamuhitaji nabii sahihi, mtu wa Mungu mwenye mafunuo ya roho mtakatifu kutoka katika mambo mengine yaliyo magumu ambayo hata pesa haiwezi kukusaidia. Kama mtu akisema kwa mtu wa Mungu, “sijui kwa nini nateseka katika maisha haya”; pale tu utakavyosema sijui kwa nini nateseka, inamaanisha unateseka kwa sababu hajui kwa nini, na hiyo ni sababu namba moja kwa nini unateseka.  Kwa hiyo kama unataka kutoka katika maisha yasiyofaa ya taabu, unatakiwa uanze kujua kwanza kwa nini unateseka.  Unatakiwa uanze kutafuta namna ya kutoka; na maana ufikiriye ni namna gani nitatoka katika hayo mateso?  Kutoka katika hali mbaya, unatakiwa ujue ni kwa namna gani! Biblia inasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa ya Mungu, kwa hivyo ni kwa kukosa maarifa ndiko kukufanyavyo uteseke.

Sababu ya pili; unateseka kwa sababu tu ya vile unavyojichukulia, inashangaza sana jinsi wale wapelelezi walivyoingia nchi ya ahadi na kupeleleza nchi na kisha walivyorudi walimtaarifu Musa ya kuwa kule tulikuwa kama panzi mbele ya macho ya wakaaji wa huko, na hali ni Mungu ndiye aliyewaficha kwa siri, walifichwa hakuna hata mmoja aliyeweza kuwaona, waliingia kwa siri na kutoka kwa siri bila kuonekana na mtu, na bado walipotoka nje eti wakasema mwachoni mwetu wenyewe tulijiona kama panzi kwao na wachoni mwao pia walituona sisi kama panzi, kwenye macho ya nani?, Hali Mungu alikuwa pamoja nao. Unajua saa nyingine u maskini, kwa sababu ya vile unavyojichukulia wewe mwenyewe, hao walikuwa wapelelezi waliofuzu kabisa kwa kazi hiyo, watu ambao walikuwa wanaweza kuingia sehemu na kutoka bila kuonekana na yeyote, na bado eti wakasema tulikuwa kama panzi mwachoni mwao, je ni nani aliwaona?, Usipende kujichukulia mwenyewe vibaya.

Sasa biblia inasema  kwa nabii, wana Israeli walikombolewa utumwani na kwa nabii, taifa la Israeli lilihifadhiwa jangwaani, kwa hiyo yote yalikuwa kwa sababu ya uwepo wa nabii na lile wingu lilikuwepo kumlinda nabii na watu wote waliokuwa naye walinufaika na wingu hilo kwa uwepo wake nabii kwao. Na kama ukisoma biblia kwa uangalifu utaona hata Gehazi alipotoka nje na kuona ukubwa wa jeshi la maadui limewazunguka alirudi na kumwambia nabii Elisha kuwa hata tumekwisha, lakini cha kushangaza nabii Elisha akamwambia’ “walio pamoja nasi ni wengi kuliko wao” na akasali ili Mungu amufungue na macho ya mfanyakazi wake yakafunguliwa naye akaona jeshi kutoka mbinguni likiwa limemzunguka nabii na ndipo mfanyakazi Gehazi naye akajiunganisha na ulinzi huo uliokuwa kwa nabii akahifadhiwa. Kwa hiyo Israeli kama taifa lilikombolewa kutoka Misri na kuhifadhiwa jangwani kwa sababu lilikuwa ni kusanyiko la kinabii chini ya Musa, nabii.

Wakati Musa alivyopewa jukumu na Mungu la kuhakikisha anakwenda na kuongea Farao juu ya wana wa Israeli, Musa akatoa sababu kwa Mungu ya kuwa ana kigugumizi hivyo hawezi kuongea vizuri, pamoja na kuwa Mungu alimshawishi  na miujiza mingi kule mlimani Sinai, hivyo Mungu kwa hasira yale maono makubwa yaliyompasa Musa pekee, Mungu akaamua kumuunganisha Haruni kaka yake Musa kwenye hayo maono ambaye kwa wakati huo alikuwa anakuja kumtafuta huko hali yuna furaha alipomuona, japokuwa ni Musa ndiye aliyekuwa kuribu na Mungu na sio Haruni na Musa alifanyika na Mungu kuwa mungu kwa Farao na kwa Haruni, hali Haruni akawa nabii wa Musa kwa Farao.  Hii ilifanyika hivi kwa namna ambayo wakati Musa alipokuwa anagugumia kuongea Haruni aweze kupakamilisha. Kwa hiyo Musa aliporudi Misri, Farao alitakiwa hata ingebidi kubadilisha dini yake kwa sababu mungu Musa alikuwa kwake sio tu kuwa kwake alikuwa akiongea na yeye Farao. Sasa ona Musa alikuwa kwanza nabii wa Mungu halafu akafanyizwa na Mwenyezi Mungu kuwa mungu kwa Farao pale tu alipokutana na Mwenyezi Mungu mlimani Sinai. Na ukumbuke pale Ibrahimu na yule Lazaro maskini kifuani mwake (Luka 16:29), Ibrahim akamwambia yule tajiri aliyekufa, ndugu zako wanaye Musa na manabii; wawasikilize hao. Kwa hiyo akina nani hao Musa na manabii, inachanganya hapo! Mungu alimfanya Musa mungu kwa Farao na kwa Haruni na Haruni kaka yake, nabii wake Musa kwa Farao (Kutoka 7:1). Hii inanihakikishia kuwa kama Musa asingejiona mwenyewe kuwa ana kigugumizi mbele ya uso wa Mungu, inamaanisha Haruni asingepaswa kuwa sehemu ya maono yale makubwa. Hata hivyo mwanzo Haruni hakuwa sehemu ya maono hayo makubwa mpaka pale Musa alipokiri ule udhaifu.
Katika maisha haya, kama Mungu ni kila kitu kwako usijichukulie kama vile huwezi jambo lolote, usipende kukiri udhaifu mbele ya uso wa Mungu ambaye ni nguvu zako (Yehova Tsori), na pia usijichukulie mwenyewe ya kuwa huwezi kufanya yaliyo mapenzi ya Mungu na kutekeleza kusudi lake kwako.

Wakati Mungu alipomfanya Musa mungu kwa Farao na kwa Haruni kaka yake na Haruni kuwa nabii wake Musa kwa Farao; Haruni alijua yakuwa alipaswa kutabiri kwa Farao na wana wa Israeli pale tu na yale tu ambayo Musa alikusudia kuyasema, kama vile neno kutoka kwa mwenyezi Mungu lilivyomjia Musa na wala sio kumjia Haruni kwa sababu katika kipindi chote hicho cha maono hayo Musa alibakia kuwa mungu kwa kaka yake Haruni (Kutoka 4:16).

Tukirejea kwa habari ya mfumo wa kitowashi; kama unataka kibali ndani ya jumba la mfalme usiharibu wala kuchakachua mbegu ya mfalme, Ukiunganishwa kwenye maono ya mtu wa Mungu unatakiwa siku zote uelewe ni mbegu ya mtu wa Mungu tu (yaani yale maono yake kama alivyopewa na Mungu) inayopaswa kujizalisha. Ni mtu wa Mungu pekee anayezalisha na sio wengine kwa niaba yake, kwa sababu maono yanayodumu milele ni yale yasiyojifitinisha yenyewe, na wala hakuna maono mengine ya tofauti katika maono yale yale yaliyo halisi aliyopokea mwanzo. Kumbuka katika huduma za kikristo; kuna walioletwa kwenye maono ya watu wa Mungu ili kusaidia katika kuyathibitisha lisianguke hata moja na kuyaendeleza, haijalishi hata kama wasaidizi hao watakuwa wanauwezo wa kuhubiri vizuri kuliko mbeba maono. Kumbuka tena Yesu anasema kuna wengine waliojifanya matowashi kwa ajili tu ya ufalme wa Mbinguni, kwa hivyo inakupasa ujitoe sadaka wewe mwenyewe na kujihasi kiroho dhidi ya mvuto wa dunia ili uwe tayari  kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

Hebu tafakari hili; mtu wa Mungu E. Makndiwa alisema baada ya kuwajulishwa waumini wake kuhusu maono ya ujenzi wa kanisa kubwa na kuwaonesha michoro kwa sinema, ndipo akamjulisha na Baba yake wa kiroho lakini baba yake huyo alivyoona akamwambia mwanangu huu ni upuuzi mtupu na kumshauri impasavyo kufanya, kwa hivyo baada ya ushauri huo wa kiroho kutoka kwa baba yake wa kiroho ikambidi kurudi tena kwa waumini walewale aliowajulisha mwanzo maono yake na kusema michoro ya ujenzi wa kanisa imebadilika kwa sababu tu kuna mtu wa Mungu  (baba yake wa kiroho) anayeona vyema zaidi yangu, mfumo wa kitowashi.

Tafakari hili tena; Mungu, japokuwa yeye ni Mungu lakini alikuja chini na kuacha vyote mbinguni na akazaliwa na mwanadamu na akanyonya maziwa ya mwandamu ili akue sio tu kunyonya, akahudhuria huduma za wanadamu, sio tu kuhudhuria huduma, alijinyenyekeza chini ya mwanadamu na kumbe yeye ni Mungu, na sio tu kujinyenyekeza, alimuruhusu mwanadamu amubatize, na hapo ndipo biblia inasema mbingu zikafunguka kwa ajili yake, nakuambia, utateseka milele kama hutajifunza kunyenyekea na kama hutatafuta mwanadamu ambaye utakwenda kwake  na kujishusha chini yake na kunyenyekea, mtu ambaye atakushika mkono na kabla hajakuinua juu atakukandamiza chini, na watu wengi wanasali na kutenda kazi chini ya mbingu zilizofungwa, mambo yao ni shida na magumu, wanasumbuliwa na pepo nyingi ziwapingazo kwa sababu tu hawako chini ya mamlaka wala hawajajinyenyekeza chini ya mtu wa Mungu, kama vile Yesu anavyomuelezea mtu mwenye imani kuu katika biblia, yule mtu aliyesema “hata mimi ni mtu chini ya mamlaka…….”.  

Je’ umeshawahi kuwaza kwa kina ni nini kinatokea unapotoa fungu la kumi kwa mtu wa Mungu au kanisa ambalo halitoi fungu la kumi kwa kanisa lolote au mtu wa Mungu yeyote yule, au unajinyenyekeza kwa mtu wa Mungu ambaye hanyenyekei kwa mtu wa Mungu yeyote yaani asiye na baba wa kiroho, yeye ndio mkubwa hakuna mkubwa juu yake (baba wa kiroho)  yaani ni Yesu tu au kwa yule asiyejua chochote kuhusu kuwa chini ya mwavuli wa baba wa kiroho, kweli hapo wewe na kanisa kunakuwa na ugumu katika kuyatenda mapenzi ya Mungu na pengine kuwa chini ya mbingu zilizofungwa na hali unaweza kuwa umejitoa kabisa kwa Yesu, kumbuka watoto wa Skeva watoto wa kuhani katika biblia hawakuwa chini ya mwavuli wa kiroho wa Paulo bali chini ya mwavuli wa kiroho wa baba yao, wakataka mamlaka ndani ya Paulo imefanye kazi kwao wakati wakifanya huduma ya ukombozi, hata kama ukitaka kutumia mwavuli wa kiroho wa mtu tofauti ndani ya huduma ya baba yako jua kuwa kuna gharama ya kulipia, kwa hivyo inaaibisha sana ukiwa na baba wa kiroho ambaye hawezi kuwakomboa watu. Saa nyingine haufanikiwi kwa sababu tu hautaki kuchukua na kuifikisha mbali zaidi mbegu ya baba yake (yale maono ndani yake).

Kuna matowashi katika falme za wanadamu, unaona raisi ana mlinzi ambaye yuko tayari kufa kwa ajili yake, yuko tayari kupokea risasi zote zilizokusudiwa kumpata raisi asiye hata na roho mtakatifu, na wala si mtakatifu lakini kwa sababu tu ana mamlaka. Je si zaidi sana ilivyotakiwa kuwa kwa watu wa Mungu walio na roho mtakatifu wa Mungu? Mfumo wa kitowashi ni mzuri hata Ufalme wa Mungu unatambua hilo, na ndio maana hata Filipo alitakiwa asimamishe kusanyiko lililokuwapo kwa ajili ya uamusho wa roho mtakatifu ili tu kumfuata towashi; ambaye alikuwa na mamlaka chini ya Kentuki malkia wa Ethiopia aliaminiwa juu ya mali na utajiri wake wote (Matendo 8:38-39). Tafakari  uzuri wa muundo huo katika kitabu cha Esta ; wakati Mfalme alivyotaka kuoa wanamke mwingine, walikusanya mabikira wote katika nchi na kuwaacha chini ya usimamizi wa towashi haggi kwa miezi kumi na mbili kabla ya kukutana na Mfalme, wakatunzwa naye na kuwa wazuri zaidi bila kuchakachuliwa. Kanisa la leo linahitaji matowashi wa kiroho ambao watakuwa tayari kutunza maono ya watu wa Mungu bila kuyaharibu au kuyapotosha, bila kuzalisha aina nyingine ya maono lakini kuyatunza na kuhakikisha yanadumu milele.

Kwa hiyo vitu vikiwa haviendi sawa unatakiwa ucheki ule muungano wako na mtu wa Mungu; je' ni kweli unaheshimu na kuitambua mamlaka? Kwa sababu kuna kitu katika maisha ambacho hata pesa haiwezi kukufanyia, unahitaji upako wa Mungu ulio ndani ya baba yako wa kiroho ili kuweka mambo sawa kwa ajili yako. Biblia inasema wapo waliojifanya wenyewe matowashi kwa ajili ya ufalme wa Mungu; je uko tayari kuacha kila kitu katika maisha yako pamoja na mke, watoto, ndugu, hata kuikataa mbegu yako kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Mephibosheth (mwana wa Jonathan) alidanganywa na mtumishi wa mfalme Daudi, wakati mfalme alipokuwa mafichoni baada ya mwanae kukaa sehemu ya kiti chake cha ufalme, na hapo Mfalme Daudi aliporudi na kumwona Mephiboshesh ya kuwa alibaki katika jumba la mfalme wala hakuambatana nae, Mfalme akamuuliza kwa nini hukuenda pamoja nami naye akasema alidanganywa  na akaongeza kuwa kwa yeye Mephibosheth yakuwa alishakufa miaka mingi iliyopita na hata hivyo akamwambia mfalme kwa nini kunitunza mpaka sasa, unaweza kuutoa uhai hata sasa kama itakufanya wewe ufurahi, wakati akiongea hayo alikuwa wakushangaza mbele ya mfalme kwa kuwa alikuwa mchafu, ananuka, nywele zimevurugika, na kama ukimuuliza kwanini alikuwa vile atakwambia kuwa aliona hakuna haja ya kuwa na raha nyumbani kwa mfalme hali mwenye jumba yuko msituni hivyo hakuwa na amani ya kula, kunywa, kuoga wala kuvaa (2 Samweli 19:24-28), Vipi kuhusu wewe?

Kwa hivyo kuwa towashi wa kiroho kwa ajili ya Ufalme wa Mbinguni. Wana wa Mungu ishi maono ya Kristo Yesu ndani yenu na heshimu watu wa Mungu (watumishi wake waaminifu) na pia utunze maono ambaye Mungu ameweka ndani yao, utahifadhiwa na kufanikiwa hakika katika jina la Yesu Kristo wa Nazareti, Ameni.

Katika andiko hili, nimehamasika kwa uvuvio wa juu sana wa Roho Mtakatifu (100%) ni somo la imani la mtu wa Mungu Emmanuel Makandiwa, Nabii wa Zimbabwe. Ni shauku yangu kuu na wewe uvuviwe na kuhamasika kwa uweza wa roho mtakatifu katika jina la Yesu Kristo wa Nazareti.

1 comment:

  1. Asante mtumishi wa Mungu, ufafanuzi wako umenifungua ufahamu zaidi na nimepokea. MUNGU akubariki

    ReplyDelete