#DHAMBI IUZAYO NAFSI KWA ADUI

Biblia inatuasa sana kuikimbie zinaa, na ya kwamba kamwe usiruhusu moyoni wako kushikwa katika tamaa itakayo kupelekea kuzini  na kisha kupoteza nafsi yako iliyo ya thamani.

Maonyo ya Biblia juu ya zinaa;

[1 Wakorintho 6:18-19]
"Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ila yeye afanyaye zinaa hutenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe. Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe". 

 [Mithali  6: 25-29]
"Usiutamani uzuri wake moyoni mwako; Wala usikubali akunase kwa kope za macho yake.
Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani.
Je! Mtu aweza kuua moto kifuani pake, Na nguo zake zisiteketezwe?
Je! Mtu aweza kukanyaga makaa ya moto, Na nyayo zake zisiungue?
Ndivyo alivyo aingiaye kwa mke wa jirani yake; Kila mtu amgusaye huyo atakuwa na hatia."

[Mithali 31:3]
"Usiwape wanawake nguvu zako; Wala moyo wako usiwape wale wawaharibuo wafalme." 

[Mithali 6: 32-33]
"Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yakeAtapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika." 
Amina.

No comments:

Post a Comment