#YESU WA NAZARETI NDIYE MKOMBOZI WA WALIO GIZANI

Yesu wa Nazareti ni Neno la Mungu lenye mamlaka yote juu ya giza,

hivyo kupitia Neno la Mungu lililojaa mamlaka ya Mungu ndiko

ukombozi kutoka gizani uliko.

Unajua hata wakati wa Musa Nabii wa Mungu kwakusaidiana na

Haruni walivyotumwa kuwakombea wana waisraeli kutoka utumwani

misri mikononi mwa Farao, Wanawaisraeli walikuwa wakifanya kazi

ya kufyatua tofali huko Gosheni mji ulikuwa umetengwa huko Misri

kwa ajili ya waisraeli kwa kazi hiyo. Walifanya kazi hiyo katika

mazingira magumu lakini pamoja na ugumu wake Mungu alikuwa nao

ndio maana ilifika wakati ulioamuliwa wao kuachiliwa huru.


Cha ajabu Musa na Haruni walipowaomba wanaisraeli kwa Farao

naye akawa mugumu kuwaachilia na zaidi ya kuwazuilia Farao pia

aliongeza kiwango cha adhabu na mazingira magumu zaidi ya utendaji

kazi hiyo na kila Musa alivyokuwa anamkemea Farao kuwaachilia

wanawaisraeli ndivyo kazi yao ilivyoongezwa ugumu jinsi ya kuitenda.

Soma Kutoka 5:6-9 inasema; Na siku ile ile Farao akawaamuru

wasimamizi wa watu, na wanyapara wao, akisema, Msiwape watu

tena majani ya kufanyia matofali, kama mlivyofanya tangu hapo; na

waende wakatafute majani wenyewe.

Lakini hesabu ya matofali waliyokuwa wakifanya tokea hapo,

wawekeeni iyo hiyo, msiipunguze hata kidogo, kwa maana ni wavivu

hao; kwa hiyo wanapiga kelele, wakisema, Tupe ruhusa twende

kumtolea Mungu wetu dhabihu, wapeni watu hao kazi nzito zaidi,

waitaabikie; wala wasiangalie maneno ya uongo. Ona pengine

wanaisraeli wangemwamini Musa, kutii maagizo yake kutoka kwa

Mungu na kuambatana naye na kusimama katika nafasi moja toka

awali hata zile adhabu zilizoongezwa za kufyatua tofali zisingedumu

na Farao asingekuwa na nguvu kuendelea kuzuia, mng’ang’anizo wake

huyo Farao ulitokana pia na hofu ya wanawaisraeli kwamba

kunakutoka kweli hapa, na kwa kuwa ule ujumbe wa Mungu kwao

kwamba sio mateka tena hawakuuamini, hivyo ililichukua Neno la

Mungu alilotamka Musa kuwa miujiza na maajabu mengi ili

kuwaaminisha kuwa ni Mungu wa baba zao ndiye aliyemtuma na

kumdhoofisha Farao kuwa anayeshindana naye si Musa bali ni Mungu

hakika muumba wa vyote ambaye ni “Nipo ambaye Nipo” yaani

Neno.

Hivyo msaada wa mtu aliyeshikwa na ufalme wa giza u katika Neno

la Mungu ambaye ndiye Yesu wa Nazareti la siivyo unavyozidi

kung’ang’ana na ufalme wa giza kuhusu uhuru wake bila yeye kujawa

na Neno ndivyo yule muathirika anavyozidi kupata vita vikali kutoka

ufalme wa giza. Kwa hiyo sala zako za kumukomboa muathirika wa

mapepo zisikome mpaka atakavyopona hakika na kuwekwa huru,

huku Neno la Mungu likifanyika msingi kwake wa maisha, kwani

yeye akijawa na Neno litampa ujasiri ambao utamuondolea hofu hivyo

naye ataweza kumpinga shetani na ufalme huo wa giza na mwisho

atakuwa huru. Kwa kuwa uhuru hauwi uhuru kama mhusika asipojijua,

Neno la Mungu pekee litamjuza mtu juu ya uhuru hivyo ni wajibu wa

mtumwa wa kristo kusimama naye imara katika imani ileile uiaminiyo

uliyomuaminisha yeye na kumthibitisha Mungu kwake aliyemkombozi

mwenye haja naye.

Na Neno lake pekee lililo ushuhuda kwake ndilo limfanyalo awe jasiri

na kutambua nafasi na sehemu yake katika ufalme wa Mungu kwa

hapo hakika ushindi utakuwa mkuu na thabiti pasipo kupitia magumu

zaidi na kufuatwafuatwa na ufalme huo wa giza au kung’ang’aniwa na

Farao.

Ndio maana katika Luka 11:24-26 Neno linasema; ”Pepo mchafu

akimtoka mtu, anazunguka jangwani akitafuta mahali pa kupumzikia.

Asipopata anasema, ‘Kwa nini nisirudi kwenye nyumba yangu

niliyotoka? Akirudi, na kuikuta ile nyumba ni safi na imepangwa

vizuri, huenda kuwaleta pepo wengine saba wachafu kuliko yeye

wakaingia na kuishi humo. Na hali ya sasa ya mtu huyo inakuwa mbaya

kuliko ya kwanza”.

Na ndio maana saa ingine najiuliza wakati wana waisraeli jangwani

wanang’atwa na nyoka na wengine kufa, maelekezo ya Bwana kwa

Musa ilikuwa ni kutengeza nyoka wa shaba na kumuweka juu ya

wote aliyethubutu kumuangalia aliwekwa huru ambaye hakutenda

hivyo alikufa, hivyo ni Neno la Bwana na maelekezo yaliyosimamiwa

na Musa na huku matokeo ya uponyaji wao ikiwa ni Bwana ndiye

atendaye. Musa aling’ang’ana na shida zao tu kwa kulifunua na kulijuza

Neno la Bwana kwao kwa kuwa alijua jawabu na matokeo ni kazi ya

Bwana ndiye afanyaye wala si yeye, Musa jukumu lake ilikuwa ni

kulisema na kuliaminisha Neno la Bwana kwao.

Hata Yesu wa Nazareti sehemu nyingi hakuhangaika na matokeo bali

Neno la Mungu alilohubiri ndio lililopelekea matokeo; ishara, ajabu

na miujiza mingi, kwa maana ingine kiu yake kuu ilikuwa ni kuufunuo

ufalme wa Mungu duniani ya kwamba watu waijue kweli ya Mungu,

waishike na kuiishi na maarifa yake yote alitumia katika hilo. Kwa

maana ni Neno la Mungu pekee ndio limuwekalo mtu huru yaani ile

kweli anayoijua ndio uhuru wenyewe lasivyo ufalme wa giza hautaacha

kumfunga.

Tunafunzwa kuwajaza Neno la Mungu, kuwafanya waliamini na kuliishi

hilo Neno kwa maarifa yote na kuwaweka katika msingi wa Neno na

kufanya nao sala mara kwa mara wale waliotangaziwa uhuru yasije

mapepo au vifungo vyovyote vya ufalme wa giza vikawashika na

kuwafunga tena, kwani kwa Yesu ndiko ziliko njia za kutoka mautini

na gizani, Amina.

http://www.slideshare.net/Recknald/depend-on-jesus-of-nazareth-man-is-a-mere-vapour

No comments:

Post a Comment