#MUOTAJI NA UZIDI OTA NDOTO NA KUZIISHI KATIKA WAKATI ULIOPO

     Hakuna ugumu wala kanuni maalum au kamili kuhusu utabiri wa ndoto. Naamini ni suala la ufahamu ingawa kuna nyingine zinachanganya kiasi kwamba utahitaji kuutafuta uso wa Mungu kwa ajili ya ufafanuzi wa ndoto hizo [Evang. Kenneth Onyene]. Kuna ndoto zingine si za kawaida bali/ila ni Ufunuo/maono [yaliyofungwa]; na kama ambavyo Mungu anatumia njia ya ndoto kuongea na sisi, tukumbuke hata shetani anatumia ndoto pia.
      Hekima, maarifa yatokanayo na neno la Mungu ndiyo yatujuzayo kuwa ni maono ya Mungu ama shetani. Ila tujue ndoto ni unabii binafsi, ni maono yaliyofungwa [closed vision]. Kumb. 29:29; inasema kwamba "mambo ya siri, ni ya Mungu wetu lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi". Mungu hawezi kukupa ndoto bila sababu ya msingi lakini hukupa ndoto kulingana na kusudi la kuumbwa kwako duniani. Mungu alimuumba Yusufu- mwana wa Yakobo ili awe kiongozi na alimpa ndoto Mwanzo 37:5-9. Mungu atakupa ndoto kukuonyesha vipaji vyako ili kukuwezesha kuvitendea kazi kama Yusufu, Mungu pia hukupa ndoto ili kukuongeza katika shughuli zako za kila siku kama Farao.
     Inawezekana kabisa ndoto zako zote zikawa kama runinga unayoangalia moja kwa moja. Lakini tukumbuke sio kila ukiota unamhitaji mtafsiri wa kutafsiri ndoto yako, unachohitaji ni kusogea kwa Mungu kwa sala mpaka ufunuliwe maana yake, kwani ni yeye aliyesababisha na kama si yeye pia utapata jibu tu. Kwa maana ndoto ni unabii binafsi ambao Mungu hukupa ili kukuwezesha kuyajua mambo ya baadaye. [Israel John O].
Tukumbuke pia Ayubu 33:14-16 inasema, “kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. Katika ndoto, katika maono ya usiku, usingizi mzito  uwajiliapo watu, katika usingizi kitandani. Ndipo huyafunua masikio ya watu, nakuyatia muhuri mafundisho yao.”

SALA:
Mungu Baba niwezeshe nami kuota na kuzitambua ndoto niziotazo na mafunuo yake yote ili niweze kuishi katika mpango na kusudi la Mungu katika jina la Yesu Kristo. Kwa maana naamini hayo yote ni wewe Mungu ndiye uyafanyaye, mara mbili, naam mara tatu, kwa mtu, ili kurudisha roho itoke shimoni [gizani], ili itiwe mwanga kwa mwanga wa walio hai [Ayubu 33:29-30], Amina.

No comments:

Post a Comment